Saudi
Arabia imewafuata makamanda wa vyeo vya juu jeshini, akiwemo mkuu wa majeshi.
Mfalme Salman pia
amefanya mabadiliko kwa makanda wa vikosi vya nchi kavu na vile vya angani.
Taarifa
hizo zilichapishwa na shirika rasmi la habari la Saudi Arabia la SPA, lakini
hakuna sababu iliyotolewa ya kufutwa kwa makamanda hao.
Mrithi wa ufalame
Mohammed bin Salman, ambaye pia ni waziri wa ulinzi anaaminiwa kuhusika kwenye
mabadiliko hayo.
Mwaka uliopita watu
mashuhuri nchini Saudi Arabia wakiwemo wanawafalme, mawaziri na wafanyabiashara
matajiri, walifungiwa kwenye hoteli ya kifahari ya Ritz-Carlto, wakati
mwanamfalme huyo aliongoza mikakati dhidi ya ufisadi na matumizi mabaya ya
mamlaka.
0 comments:
Post a Comment