Mahakama
ya Hakimu Mkazi Mbeya imewatia hatiani mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi
maarufu Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Emmanuel
Masonga, na kuwahukumu kifungo cha miezi mitano jela.
Hukumu hiyo imetolewa leo Februari 26 2018
na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Michael Mteite.
Sugu na Masonga wamehukumiwa kwa kosa la
kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.
Wawili hao wanadaiwa kutenda kosa hilo
kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Desemba 30 2017 eneo la Uwanja wa Shule
ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.
0 comments:
Post a Comment