Monday 26 February 2018

SUGU, MASONGA WAHUKUMIWA JELA MIEZI MITANO.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya imewatia hatiani mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Emmanuel Masonga, na kuwahukumu kifungo cha miezi mitano jela.

Hukumu hiyo imetolewa leo Februari 26 2018 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Michael Mteite.
Sugu na Masonga wamehukumiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Wawili hao wanadaiwa kutenda kosa hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Desemba 30 2017 eneo la Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

0 comments:

Post a Comment