Mwanamke
amegundua nyoka mwenye sumu kali ndani ya mkebe ambao mtoto wake anatumia
kebeba chakula cha mchana nchini Australia.
Nyoka huyo
aligunduliwa amejificha kwenye kifuniko, wakati mama huyo alikuwa akiweka
chakula kwenye mkebe huko Adelaide, kulingana mshikaji nyoka Rolly Burrel.
Bw Burrel
alisema almshauri mwanamke huyo kufunika mkebe na kuupeleka nje wakati alimpigi
simu kumuomba usaidizi.
Alimtaja
nyoka huyo kama eastern brown, mmoja wa nyoka wenye sumu kali zaidi duniani,na alisema
nyoka huyo alitolewa salama.
Mshikaji nyoka huyo
alisema kuwa anashuku nyoka huyo aliiangia kwennye mkebe huo kwa sababu labda
ndiko alipata giza.
Nyoka wa
aina hiyo hupatikana maeneo ya pwani mwa Australia na amehusika na vifo 23
tangu mwaka 2000 kwa mujibu wa utafiti.
0 comments:
Post a Comment