Monday 13 November 2017

ASKARI WALIOBAKA WATOTO WA MIEZI 18 KIZIMBANI DRC…

Wanajeshi 18 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, wamepandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza wakikabiliwa na kesi ya ubakaji wa halaiki wa watoto.

Wanajeshi hao wanadaiwa kuwabaka watoto wa kike 46 katika kijiji cha Kavumu, na kwamba kati yao walikuwemo wenye umri hadi miezi 18 tu.
Watuhumiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo kati ya mwaka 2013 na 2016 kwa sababu za imani ya kishirikina, kuwa damu ya wasichana bikira ingeweza kuwapa nguvu ya ajabu na ulinzi.
Hata hivyo kiongozi wa wanajeshi hao anayetambulika kwa jina la Frederic Batumike na wenzake, walikana mashtaka hayo.

Makundi ya haki za binadamu yanaamini ufunguzi wa kesi hizo, utamaliza utamaduni wa ubakaji unaochukuliwa kama sehemu ya nguvu ya kivita nchini humo.

0 comments:

Post a Comment