ina mpya ya vimelea vya ugonjwa wa kisonono au "gono" ambavyo vinahimili dawa (resistant to drugs)
zinazotumika kutibu ugojwa huu imegundulika duniani. Taarifa
iliyotolewa na shirika la afya duniani (WHO) hivi karibuni imesema,
ugonjwa wa kisonono unaoathiri mamilioni ya watu ulimwenguni umeanza
kuwa sugu dhidhi ya dawa zinazotumiwa kuutibu na hivyo kuna hatari ya
kutoweza kutibika kabisa.
Shirika
la afya duniani limetoa wito kwa serikali na madaktari kuongeza
ufuatlijiaji wa aina hii ya kisonono kutokana na ugonjwa wa
kisonono kuwa na athari nyingi kama mcharuko (inflammation), ugumba, matatizo wakati wa ujauzito na hata vifo vya kina mama wajawazito.
“Aina
hii mpya ya vimelea vya kisonono vinaonyesha usugu dhidhi ya dawa zote
za antibiotiki tunazotumia dhidhi yake ikiwemo dawa za jamii ya
cephalosporins ambazo ni dawa za mwisho katika kutibu ugonjwa wa
kisonono, “ alisema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan, mmoja wa wanasayansi
wa shirika la afya duniani katika kitengo cha magonjwa ya zinaa.
Miaka
michache ijayo, aina hii mpya ya kisonono itakuwa sugu dhidhi ya dawa
zote ambazo tunazo saizi “aliendelea kusema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan
wakati wa mahojiano na shirika la habari la The Associated Press kabla
WHO haijatangaza rasmi hatua na mwongozo mpya wa kukabiliana na tishio
la aina hii mpya ya kisonono.
Inakisiwa
watu milioni 106 ulimwenguni kote huathiriwa na ugonjwa wa
kisonono kila mwaka.Ugonjwa wa kisonono pia huongeza hatari ya kupata
maambukizi ya ugonjwa wa Virusi vya Ukimwi (VVU).
“Ugonjwa
sugu wa kisonono sio tatizo la bara la Ulaya au Afrika pekee bali ni
tatizo la dunia nzima kwa sasa,’” alinukuliwa akisema Dk. Manjula
Lusti-Narasimhan.
Kwa
mara ya kwanza, vimelea sugu vya ugonjwa wa kisonono dhidhi ya dawa
aina ya cephalosporins viliripotiwa katika nchi ya Japan, ikifuatiwa na
Uingereza, Hongkong na Norway.
Wanasayansi
wanaamini matumizi mabaya ya dawa aina ya antibiotiki pamoja na uwezo
wa vimelea vya ugonjwa wa kisonono kubadilika na kuzoea mazingira mapya
ndio chanzo kikuu cha kutokea kwa ugonjwa sugu wa kisonono na hivyo muda
si mrefu ugonjwa huu utakuwa janga kubwa dunia nzima kama hatua za
haraka hazitachukuliwa. Kuna uwezekano wa vimelea hivi sugu vya
kisonono vinasambaa kwa sasa duniani bila kuweza kugundulika kutokana na
nchi nyingi kutokuwa na ufuatiliaji na utunzaji kumbukumbu mzuri wa
wagonjwa wake.
Shirika
la afya duniani limesema nchi zinatakiwa kuongeza ufuatiliaji wa
wagonjwa wake pamoja na kudhibiti matumizi holela ya dawa za antibiotiki
mpaka pale taarifa kamili za ugonjwa huu zitakapojulikana.
“Elimu
ya masuala ya kujamiana pamoja na matumizi sahihi ya mipira ya kondomu
inahitajika ili kutokomeza kabisa ugonjwa huu sugu wa kisonono. Hatuwezi
kuutokomeza kabisa ugonjwa huu bali tunaweza kuzuia usambaaji
wake,”alisema Dk. Manjula Lusti-Narasimhan.
0 comments:
Post a Comment