Friday 21 August 2015

Marufuku kupeana mikono Dar…

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik, amewataka wakazi wa jijini hilo kuchukua hadhari za kiafya ikiwamo kuacha kusalimiana kwa kushikana mikono kutokana na mlipuko wa kipindupindu ambao mpaka sasa umeshawapata watu 56, kati yao watatu wamefariki dunia.

Akizungumza jana ofisini kwake mbali na kushikana mikono, Sadik amewataka wananchi kuacha kunywa maji ya viroba maarufu kama “maji ya Kandoro” na juisi za mitaani ili kupunguza uwezekano wa kupata ugonjwa huo.
Amesema ugonjwa huo ulilipuka Agosti 15 baada ya mtu mmoja kufariki dunia katika Hospitali ya Mwananyamala.

Amesema idadi ya wagonjwa imeongezeka hadi kufikia 56, lakini mpaka sasa wamebaki wagonjwa 36 katika kituo maalumu kilichofunguliwa Mbagala baada ya wengine kutibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani.

0 comments:

Post a Comment