Siku za hivi karibuni baadhi ya maeneo
Stori za joto kuongezeka,zimekuwa zikichukua nafasi kubwa sana, nikukumbushe tu
kwamba ilianza kule Dubai ambapo joto lilipanda mpaka kufikia nyuzi 38, tukasikia Uingereza nako nyuzi joto nako zilipanda
hadi kufikia 40 lakini kule india na
kwenyewe joto lilipamda hadi kufikia nyuzi 45.
Sasa stori toka nchini Italy ni
kwamba nyuzi joto limeongezeka kufikia nyuzi 37C, na hii imepelekea matukio na athari za jua yamekuwa yakiripotiwa sana nchini umo.
Moja ya stori toka huko ni
hii ya sehemu za urembo wa gari dogo lililokuwa limeegeshwa, kuyeyuka kutokana
na joto kali la jua.
Tukio lilinaswa kwenye picha na video na mtalii mmoja aliyekuwa anatoka
hotelini kuelekea beach, na kisha kushangazwa kuona uji uji mzito unidondoka
kutoka kwenye gari hilo, alipolikaribia gari hilo aligundua kuwa gari lilikuwa
linayeyuka kutokana na joto kali la jua
Kitu hiki kimewashangaza watu wengi huku vyombo vingi vya usalama
nchini humo, vimewaomba watu kupunguza kutoka nje na kwenda baharini na kufunga
viyoyozi vitakavyowasaidia kupunguza joto.
0 comments:
Post a Comment