Utawala
nchini Indonesia unasema kuwa hali mbaya ya hewa imewalazimu kusitisha
oparesheni za kuwatafuta manusura wa ajali ya ndege ambayo ilianguka siku ya
Jumapili katika milima iliyo mashariki mwa Papua.
Ndege hiyo ilikuwa imebeba abiria
54 na karibu dola nusu milioni pesa taslimu.
Mkuu wa posta katika mji mkuu wa
Papua wa Jayapura aliambia BBC kuwa pesa hizo zilizokuwa ndani ya mifuko minne
ilikuwa sehemu ya mchango wa serikaki kwa watu maskini.
Shirika moja linalohusika na
kusaka ndege hiyo linasema kuwa limegundua yaliyo mabaki ambao ni umblai ya
kilomita 50 kutoka mahala ndege hiyo ilitakiwa kutua.
0 comments:
Post a Comment