Baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu bila timu,
golikipa mkongwe na mahiri Juma Kaseja August
19 amesaini mkataba wa miezi sita wa kuitumikia klabu yaMbeya City kutoka Jijini Mbeya.
Mkataba wa Juma
Kaseja wa kujiunga na klabu ya Mbeya
City umesainiwa mbele ya
meneja wake mpya Athumani Tippo.
Kabla ya kusaini mkataba na Mbeya City, Juma Kaseja alikuwa
nje ya uwanja kwa kipindi cha zaidi ya miezi nane, baada ya kuingia katika
mgogoro wa kimkataba na iliyokuwa klabu yake ya zamani ya Yanga nakufanya kesi hiyo kutinga
mahakamani.
0 comments:
Post a Comment