Unywaji
kidogo wa pombe hadi chupa moja kwa siku kwa wanawake na chupa mbili kwa
wanaume, unaweza kusababisha hatari ya kupata saratani kulingana na watafiti.
Makala moja ya Uingereza
ilichambua utafiti mkubwa kutoka nchini Marekani uliofanyiwa zaidi ya watu
100,000.
Wataalamu wanasema kuwa matokeo
hayo yanatuma ujumbe wa kiafya kuwa watu wanahitaji kupunguza kiwango cha pombe
wanachokunywa na mara nyinge hata kuwa na siku ambazo hawanywi pombe.
Mara nyingi inahitajika kuwa wanaume wanaweza kunywa
zaidi ya chupa tatu kwa siku na wanawake zaidi ya chupa mbili au tatu lakini
huenda viwango hivyo vikafanyiwa marekebisho.
Watafiti hao pia waligundua kuwa
hatari inayotoka na unywaji wa pombe hasa satarani ya matiti iliongezeka hata
kwa kunywa chupa moja ya pombe kwa siku.
0 comments:
Post a Comment