Bondia
Floyd Maywether atapanda tena ulingoni mwezi Septemba 12 mwaka huu kuzipiga na
Andre Berto.
Floyd atajaribu kuifikia rekodi
ya bondia Rocky Marciano,ya kupigana mapambano 49 pasipo kupoteza.
Berto ameshinda mapambano 30 huku akipoteza mapambano
matatu.
Bondia mwingereza Amir Khan
alikua na matumaini ya kuzipiga na Mayweather, baada ya kumpiga Chris Algieri mwezi
Juni.
Mayweather alieleza baada ya
pambano lake na Manny Pacquiao, kuwa atacheza pambano moja tu la mwisho kabla
ya kustaafu mchezo wa masubwi.
0 comments:
Post a Comment