Michuano
ya kumi na nne ya Kombe la dunia la mchezo wa pete itaanza kutimua vumbi leo
katika jiji la Sydney nchini Australia.
Jumla ya michezo sitini na minne
itacheza katika siku kumi za michuano hiyo ambapo timu kumi na sita zitachuana
kuwania ubingwa wa dunia.
Viwanja viwili vya Allphones na
City Olympic Park ndio vitatumika katika michuano hii.
Katika kundi A kuna wenyeji
Australia, New Zealand , Barbados,Trinidad & Tobago.
Kundi B lina timu za
England,Jamaica,Scotland na Samoa.
Kundi C Afrika Kusini,Malawi,Sri
Lanka, Singapore.
Kundi D kuna timu za Fiji, Wales
, Zambia, Uganda.
0 comments:
Post a Comment