Binti wa miaka kumi na mmoja nchini
Paraguay aliyedai kubakwa na baba yake wa kambo, amejifungua mtoto wa kike
baada ya mamlaka nchini humo kumzuia asitoe ujauzito aliokua nao.
Madaktari
katika mji mkuu wa Asuncion wamesema kuwa,binti huyo na mtoto wake
aliyejifungua kwa njia ya upasuaji wanaendelea vizuri.
Tukio
hilo limesababisha utata mkubwa nchini humo na katika mitandao ya kijamii,
Paraguay ni taifa linaloamini zaidi katika Ukatoliki, ambapo mwanamke
anaruhusiwa kutoa mimba pale tu afya yake inapokuwa hatarini.
Binti
huyo alibakwa alipokua na umri wa miaka kumi pekee,na Baba yake wa kambo mwenye
miaka arobaini na miwili yupo rumande,akisubiria kutajwa kwa kesi yake wakati
huo huo baba huyo amekanusha kuhusika katika tukio hilo.
0 comments:
Post a Comment