Uamuzi huo wa majaji saba katika
mahakama hiyo umetolewa baada ya wanaharakati wa haki za wanawake kuwasilisha
kesi mahakamani wakisiema kuwa utamaduni huo unawanyima wanawake haki zao.
Jaji mkuu wa Uganda Bart Magunda
Katureebe amesema kuwa ikiwa utamaduni huo utaruhusiwa kuendelea itakuwa na
maana kuwa wanawake ni kama bidhaa zinazouzwa sokoni.
Lakini idadi kubwa ya majaji hao
walikubaliana na uamuzi kwamba utamaduni wa utoaji mahari unapaswa kuendelea na
kwamba haukiuki katiba.
Hata hivyo mmoja wa majaji hao
alisema kuwa utamaduni huo unawadhalilisha wanawake na kwamba mahakama inapaswa
kulifanya swala la ulipaji mahari kuwa chaguo na wala sio sharti.
0 comments:
Post a Comment