Mmlaka ya chakula na Dawa TFDA, imeatoa ripoti ya mwaka wa fedha
kuhusu bidhaa mbalimbali zilizokamatwa na kuteketezwa kwa mujibu wa sheria
na hatua zilizochukuliwa.
Mkurugenzi wa TFDA Hitti Sillo amesema katika mwaka wa fedha
wamekamata na kuteketeza vipodozi ambavyo vimepigwa marufuku tani 16.61
ambazo thamani yake ni shilingi milioni 44.2.
Amesema
kazi hiyo ni endelevu kwa kuwa TFDA ipo sehemu mbalimbali nchini, na wakaguzi
wake wapo kuanzia bandarini na katika viwanja vya ndege ambapo ndipo hukamataa
bidhaa nyingi.
Amesema
miaka mitatu iliyopita udhibiti umeimarika sana, ndio maana matukio mengi ya
kukamatwa kwa watu ambao wanaingiza vipodozi hatari kinyume cha sheria
wanakamatwa wakiwa mipakani.
0 comments:
Post a Comment