Utafiti
uliofanywa kwa zaidi ya watu laki tano, umeeleza kuwa watu wanaofanya kazi kwa
saa nyingi, wako hatarini kupata kiharusi.
Takwimu zilizochapishwa kwenye jarida la kitabibu la Lancet,
linaonyesha upo uwezekano wa ongezeko la hatari ya ugonjwa huo kwa watu
wanaofanya kazi zaidi ya muda wa kawaida.
Wataalam wanasema watu wanaofanya
kazi kwa saa nyingi zaidi, wawe na utaratibu wa kupima kiwango cha msukumo wa
damu.
Wataalamu wanasema kufanya kazi
kwa muda mrefu zaidi kuliko kawaida, na kukaa kwa muda mrefu ni mbaya kwa afya
na ongezeko la hatari ya kupata kiharusi.
Daktari Kivimaki ameuambia
Mtandao wa Habari wa BBC kuwa,watu wanapaswa kuwa makini na afya zao, kuangalia
mtindo wao wa maisha na kuhakikisha wanapima vipimo vya damu kuepuka shinikizo
la damu.
0 comments:
Post a Comment