Tuesday 18 August 2015

Wafanyakazi sekta ya umeme Madagascar wagoma…….

Wafanyakazi wa shirika la umeme nchini Madagascar wamegoma kazi kulalamikia hali mbaya ya kimaisha.


Mgomo huo ambao umekuja baada ya ule wa wafanyakazi wa shirika la ndege nchini humo, ulianza jana Jumatatu ambapo wafanyakazi hao walilalamikia mshahara wa chini wanaolipwa na serikali.

Migogoro ya kijamii na migomo ya kila mara katika sekta tofauti za serikali, ni changamono nyingine ambayo imewasukuma wabunge kuzidisha mashinikizo kwa serikali ya Rais Hery Rajaonarimampianina, ambapo hivi karibuni bunge la nchi hiyo lilipitisha kwa wingi wa kura muswada wa kutokuwa na imani na rais huyo, kwa madai ya kukiuka katiba na kutokuwa na uwezo wa kuongoza nchi.

Hii ni katika hali ambayo tayari walimu wa shule za msingi na wale wa vyuo vikuu na kadhalika wafanyakazi wa taasisi za kitaifa nchini Madagascar, wametangaza kuanza mgomo wao siku chache zijazo.

Mgomo wa mwezi mmoja wa wafanyakazi wa shirika la ndege ambao ulifanyika kuanzia tarehe 17 Juni mwaka huu, ulipelekeakuvunjwa safari za ndege na hivyo kuathiri kwa kiasi kikubwa uchumi hususan katika sekta ya utalii.


Weledi wa mambo wanatabiri kuwa, kuendelea migomo hiyo, kunaweza kumfanya Rais Hery Rajaonarimampianina kujiuzulu.

0 comments:

Post a Comment