Wednesday 5 August 2015

Takriban watu 20 wapoteza maisha India…………

Treni zilipotea njia na kutumbukia mtoni
Treni mbili zimekosea njia huko nchini India na kutumbukia katika mto nchini humo.Treni hizo za abiria zilitumbukia katika mto uliokuwa umefurika, kufuatia mvua kubwa katika Jimbo la Madhya Pradesh.
Shirika la habari la Associated Press, limemnunukuu mmoja wa waokoaji akisema kuwa wamehesabu maiti 20.
Zaidi ya abiria 250 wameokolewa, baada ya mabehewa sita kutumbukia mtoni
Wakuu wa shirika la Reli la India wanasema kuwa,ajali hiyo ilitokea usiku wa manane kuamkia jumatano.

Anil Saksena ni msemaji Shirika la Reli la India, amesema Treni moja ilitoka katika njia yake huku nyingine ikifuatia nyuma yake katika njia ya kupishana, Treni zilipoteza mwelekeo kutokana na mafuriko.

0 comments:

Post a Comment