Shirika la habari la Associated
Press, limemnunukuu mmoja wa waokoaji akisema kuwa wamehesabu maiti 20.
Zaidi ya abiria 250 wameokolewa,
baada ya mabehewa sita kutumbukia mtoni
Wakuu wa shirika la Reli la India
wanasema kuwa,ajali hiyo ilitokea usiku wa manane kuamkia jumatano.
Anil Saksena ni msemaji Shirika
la Reli la India, amesema Treni moja ilitoka katika njia yake huku nyingine
ikifuatia nyuma yake katika njia ya kupishana, Treni zilipoteza mwelekeo
kutokana na mafuriko.
0 comments:
Post a Comment