Rais
wa zamani wa Cuba Fidel Castro ametimiza umri wa miaka 89 kwa kuandika barua ya
wazi kwa taifa lake.
Barua hiyo ilichapishwa katika
gazeti la serikali la Granma,ambapo hajazungumzia lolote kuhusu ufunguzi wa
ubalozi mpya wa Marekani jijini Havana,utakavyofanya kazi na waziri wa mambo ya
nje wa Marekani John Kerry.
Badala yake ameituhumu Marekani
kwa kuisababishia hasara ya mamilioni ya dola,baada ya miaka mingi ya vikwazo
vya biashara baina ya nchi hizo mbili.
Lakini amezungumzia maridhiano ya
kihistoria kati ya nchi yake na Marekani.
0 comments:
Post a Comment