Boti moja
iliyokuwa imebeba abiria 23, imegongana na mtumbwi wa wavuvi na kuzama katika
ziwa Victoria Magharibi mwa Kenya.
Taarifa za awali zilikuwa zimetoa idadi hiyo kuwa 200, lakini
maafisa wa usalama nchini Kenya wamethibitisha kuwa idadi ya abiria kwenye boti
hiyo ilikuwa 23 na watu 21 wameokolewa.
Miili ya watoto
wawili imepatikana ikielea kwenye ziwa hilo.
Afisa wa usalama nchni nhumo ameiambia BBC kuwa, waliwaokoa
watu 14 walipowasili katika eneo la tukio kabla ya kuwanusuru wengine saba
waliporejea mara ya pili.
Kwa mujibu wa walionusurika, boti hilo lililokuwa limewabeba
abiria liligonga mtumbwi wa wavuvi kisha zote mbili zikazama majini.
Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa kumi na mbili asubuhi hii
leo, ajali hiyo imetokea karibu na visiwa viwili vidogo ndani ya ziwa Victoria
viitwavyo Kiwa na Remba Magharibi mwa Kenya.
Boti hiyo
iliyokuwa na abiria ilikuwa inaelekea Sori kutoka kisiwa cha Remba.
0 comments:
Post a Comment