Kimengenyo (enzyme)
ambacho ni protini aina ya CYP2E1 kimegundulika kuwa ndio chanzo
kinachochangia wanawake kupata saratani ya matiti kwa wanawake
wanaotumia vilevi. Kwa muda mrefu wanasayansi walikuwa wakitafuta
uthibitisho wa uhusiano wa kunywa pombe na saratani ya matiti, lakini
sasa wameweza kupata uhusiano huo. Protini hii hupatikana kwenye matiti
ya wanawake na hivyo kuwaweka kwenye hatari kubwa ya kupata saratani ya
matiti kama watakuwa wanakunywa sana vilevi kama pombe, whiskey, wine na nk.
Utafiti
uliofanywa na chuo kikuu cha Autonomous University of the State of
Morelos cha nchini Mexico, umeonyesha ya kwamba protini hiyo ya aina ya
CYP2E1 inauwezo wa kukivunja vunja kilewesho (ethanol) na kusababisha kutolewa kwa kemikali hatari zinazojulikana kama free radicals.
Watafiti
hao wamesema ugunduzi wao utasaidia katika kuvumbua kipimo
kitakachosaidia kujua ni wanawake gani walio na protini hii ya CYP2E1 na
hivyo kuwasaidia kujikinga dhidhi ya saratani ya matiti.
Kemikali
hizi hatari uhusishwa na kutokea kwa baadhi ya magonjwa kama saratani
mbalimbali, ugonjwa wa kisukari, uharibifu wa mishipa ya damu aina ya
ateri (arteries), kuchangia mtu kuzeeka na nk.
Swali
kuu walilojiuliza watafiti wakati wa utafiti huo ni , Je kuwa na
protini hii ya CYP2E1 kwa wingi huchangia mwanamke kupata
ethanol-induced toxicity na hivyo kumhatarisha kupata saratani ya
matiti?
Matokeo
yetu yalionyesha ya kwamba seli za kutoka katika matiti ya mwanamke
(mammary cells) zilizowekwa kilewesho cha aina ya ethanol, hutoa
kemikali hatari kwa wingi, husababisha kuwepo kwa oxidative stress,
huharakisha ufanyaji kazi wa seli na hivyo kuongeza kiwango cha ukuaji
wa seli hizi kwa wingi na kusababisha saratani ya matiti” alisema
Profesa Maria de Lourdes Rodriguez-Fragoso, kutoka chuo kikuu cha The
Autonomous University of the State of Morelos cha nchini Mexico.
Uchunguzi
uliofanywa kutoka kwenye tishu za matiti ya wanawake wenye afya njema
ambao wamefanyiwa upasuaji wa kukuza matiti yao umeonyesha viwango
tofauti vya protini hii katika wanawake hawa.
“Hii
inamaanisha ya kwamba wanawake wanatafautiana kwa umengenywaji wa pombe
na hivyo inabidi kila mwanamke kuchukua hatua tofauti katika kupunguza
uwezekano wa kupata saratani ya matiti” Alisema tena Profesa Maria de
Lourdes Rodriguez-Fragoso.
Protini hii ya aina ya CYP2E1 hupatikana katika seli za matiti ya mwanamke zinazojulikana kama mammary epithelial cells
ambapo pia ndio chanzo cha seli/chembechembe nyingi za saratani ya
matiti na kusababisha watafiti hao kuanza kushuku uhusiano wake na
saratani ya matiti.
Ili
kuthibitisha shauku yao kwamba protini hii husababisha saratani ya
matiti, watafiti hao walichukua tishu za matiti zilizo na viwango
tofauti vya CYP2E1 na kuziweka kwenye pombe. Matokeo yalionyesha ya
kwamba seli zenye kiwango kidogo cha protini aina ya CYP2E1
hazikuathiriwa sana ikilinganishwa na seli ambazo zilikuwa na kiwango
kikubwa cha protini hiyo.
Utafiti
huu ni ushindi mkubwa katika vita dhidhi ya saratani ya matiti kwani
utasaidia kupunguza kiwango cha saratani hii kwa wanawake
0 comments:
Post a Comment