Shirika la Anga za Juu la Marekani (Nasa) leo linatarajiwa kutangaza
ugunduzi "mkubwa" kuhusu mambo yaliyomo "nje ya mfumo wetu wa
jua".
Hafla ya kutangaza ugunduzi
huo itapeperushwa moja kwa moja kupitia runinga ya Nasa na katika mtandao wa
shirika hilo mwendo wa saa kumi na mbili jioni (GMT) ambazo ni sawa na saa tatu
Afrika Mashariki Jumatano jioni.
Habari kuhusu tangazo hilo pia zitachapishwa katika
jarida la kisayansi la Nature na baadaye katika Reddit AMA (Ask Me
Anything/Niulize Chochote).
Je, ni baadhi ya mambo gani wataalamu
Nasa wanaweza kuwa wanataka kuwatangazia watu?
![]() |
Nasa watatangaza kugunduliwa kwa viumbe hai anga za juu? |
Kuna
uwezekano kwamba amegundua viumbe wanaoishi anga za juu?
Hili ni
suala la kwanza watu kulifikiria, na tayari kunao wanaolijadili kwenye Twitter.
Lakini
usisikitike sana iwapo hakutakuwa na ugunduzi wowote kama huo.
Moja ya
viashiria vya kuwepo na viumbe hai anga za juu au katika sayari nyingine ni
uwepo wa maji.
Mwaka
2015, Dkt Joe Michalski wa Makumbusho ya Historia ya mambo Asilia London
alisema, "Duniani, popote unapopata maji, huwa kuna uhai."
Wakati
huo, Nasa walikuwa wanatangaza kugunduliwa kwa kiowevu juu ya Mars. Maeneo
yenye kiowevu hicho Mars yalitajwa kuwa pahala pazuri pa kutafuta viumbe walio
hai, kwa hivyo huenda Nasa wamegundua maji katika sayari nyingine.
Lakini
wanasayansi pia wamekiri kwamba itachukua muda kuyachunguza maji ya Mars kwa
karibu na kwa kina zaidi.
Kuna
makubaliano ya kimataifa ya kuzuia kufika kwa vyombo vya anga za juu maeneo ya
Mars yanayodhaniwa kuwa na maji bila kutibiwa vyema, kuzuia kuingizwa kwa sumu
au viumbe ambao huenda wakavuruga usafi au kuingilia yaliyopo maeneo hayo.

Nasa wamekuwa wakisema kuna uwezekano wa kuwepo maji Mars

0 comments:
Post a Comment