Wednesday, 1 February 2017

MPANGO ATAJA KINACHOKWAMISHA UKUAJI WA UCHUMI…..

Serikali imesema matokeo ya ukuaji wa pato la taifa kwa mwaka 2016 yalitarajiwa kuwa 7.2% lakini kwa uchambuzi uliofanywa na serikali kwa kushirikiana na shirika la fedha duniani IMF unaonesha kuwa ukuaji wa uchumi uliotegemewa unaweza usifikiwe.


Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mipango wakati akiwasilisha kauli ya serikali bungeni kuhusu mwenendo wa hali ya uchumi wa taifa ilivyo na kuongeza kuwa matarajio ya sasa ni kufikia ukuaji wa wastani wa asilimia 7.0.

Amesema kuzorota kwa ukuaji wa uchumi nchini umetokana na kwamba nchi za Jumuiya ya Ulaya na China ambao ni wabia wakubwa wa Tanzania kibiashara na uwekezaji ndiyo kumechangia kupunguza matarajio ya awali ya kasi ya ukuaji wa uchumi nchini.

Wakati huohuo Dkt. Mipango amesema uamuzi wa serikali kuzitaka taasisi za umma kufungua akaunti za mapato benki kuu ni sababu pia ya kupungua kwa ukwasi katika uchumi wa nchi.


Tizama vieo hapo chini..

Related Posts:

  • WANAOTOA SIRI ZA SERIKALI MTANDAONI KUTUPWA JELA MIAKA 20.. Serikali imetoa onyo kwa watumishi wa umma wanaotoa siri za serikali na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii kuwa watachukuliwa hatua za kisheria. Onyo hilo lilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Waziri wa Ofisi ya R… Read More
  • TUNDU LISSU ATEMA CHECHE…. Wakati Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu, akiwa bado anakabiliwa na kesi kadhaa za uchochezi, amefytuka tena na kutoa maneno mazito juu ya viongozi wa Serikali, huku akisema kwa … Read More
  • WAUMINI WAWILI WAFA MAJI WAKIBATIZWA.. Waumini wawili wa Kanisa Siloam wamekufa maji wakibatizwa katika Mto Ungwasi wilayani Rombo baada ya mmoja wao kupandisha mapepo na kuwatumbukiza majini wenzake. Mkuu wa Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro Agnes Hokororo… Read More
  • MUUGUZI AMDUNGA BINTI SINDANO NA KUMBAKA…… Muuguzi anayefanya kazi Kituo cha Afya Kata ya Igurubi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Damian Mgaya (26) anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma ya kumbaka binti wa miaka 18 mkazi wa kitongoji cha Mwagala B, Kijiji cha Mwagala.… Read More
  • ROONEY AITEKA DAR………   Mshambuliaji mpya wa Everton Wayne Rooney, amekuwa kivutio wakati msafara wa timu hiyo ulipowasili jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Everton iliyowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa (JNIA) ilipokelewa na Wa… Read More

0 comments:

Post a Comment