Thursday, 9 February 2017

TUNDU LISSU AGOMA KULA, ADAI MPAKA AFIKISHWE MAHAKAMANI..

Wakati Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu akigoma kula hadi afikishwe mahakamani, wakili wake amepeleka maombi Mahakama Kuu kuomba apewe dhamana baada ya polisi kuendelea kumshikilia kwa siku ya tatu.

Wakili wa mbunge huyo Peter Kibatala amesema kuwa, mteja wake amefikia hatua hiyo, baada ya Jeshi la Polisi linalomshikilia kumnyima dhamana bila sababu.
Kibatala amesema hakuna sababu za msingi za kumnyima dhamana mteja wake, na tangu jana Lissu hajala na amesema hatakula hadi afikishwe mahakamani.
Amesema mteja wao analalamikia kuanzia ukamatwaji wake ulipoanza, alipokamatwa eneo la Bunge bila Spika kuwa na taarifa.

Kibatala amesema polisi waliokwenda kumkamata aliwatambua njiani na alikamatwa bila kuwapo kibali cha kukamata (arrest warrant)

Related Posts:

  • TUNDU LISSU AGOMA KULA, ADAI MPAKA AFIKISHWE MAHAKAMANI.. Wakati Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu akigoma kula hadi afikishwe mahakamani, wakili wake amepeleka maombi Mahakama Kuu kuomba apewe dhamana baada ya polisi kuendelea kumshikilia kwa siku ya tatu. Wa… Read More
  • MAJAJI WAJINOA MAHAKAMA YA UFISADI…!! Jaji Mkuu wa tanzania Mohamed Chande amesema kuwa, jopo la majaji linatarajiwa kuingia darasani ili kujifunza sheria mpya ya kuendesha kesi za ufisadi.  Kesi hizo zitakuwa zinaendeshwa katika Mahakama Kuu Kite… Read More
  • LEMA AZIDI KUKWAMA GEREZANI.. Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, imetupa pingamizi la mawakili wa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema la kuitaka isisikilize kesi ya kuhamasisha maandamano ya Ukuta, bali kwanza ifikishwe Mahakama ya Katiba. Lema, amb… Read More

0 comments:

Post a Comment