Thursday 16 February 2017

WALIOONGOZA MGOMO WA MADAKTARI WAACHIWA HURU

Mahakama ya Rufaa nchini Kenya imeamuru kuachiliwa huru mara moja kwa viongozi wa chama cha wauguzi na madaktari nchini humo waliohukumiwa kifungo cha mwezi mmoja jela.


Viongozi hao saba walifungwa Jumatatu wiki hii baada ya kupatikana na hatia ya kutotii amri ya mahakama ya kuwataka kumaliza mgomo wa madaktari ambao umedumu kwa zaidi ya miezi miwili sasa.

Viongozi hao wametakiwa kuhakikisha suluhu ya mgomo huo inapatikana katika kipindi cha siku saba.
Mazungumzo ya kutafuta suluhu yataongozwa na Chama cha Wanasheria Kenya (LSK) na Tume ya Taifa ya Haki za Binadamu (KNHCR).
Madaktari wamekuwa wakiitaka serikali kuheshimu makubaliano ya mwaka 2013 ya kuwaongezea mishahara na kuboresha mazingira ya utendaji kazi hospitalini

Wamekataa mshahara walioongezewa na serikali wa asilimia 40 wakisema kuwa ni wa chini kuliko ule walioafikiana mwaka 2013.


0 comments:

Post a Comment