Wednesday 22 February 2017

KASHMIR:MARUFUKU MATUMIZI YA ANASA…..

Serikali ya Jimbo la Kashmir nchini India imeweka zuio dhidi ya gharama za anasa.
Wazazi wa bibi harusi watapigwa marufuku kualika zaidi ya wageni mia tano, au mia nne ikiwa mtoto wa kiume atakuwa anaoa.

Idadi ya aina ya vyakula kwenye sherehe itakuwa saba, huku mziki wa sauti ya juu na fataki vitapigwa marufuku.
Serikali ya kashmir imesema imechukua hatua hiyo, baada ya kuwepo kwa malalamiko ya watu kuhusu matumizi makubwa wakati wa sherehe na kelele zinazowakera wengine.

Amri hizo zitaanza kufanya kazi mwezi Aprili mwaka huu.

0 comments:

Post a Comment