Friday 10 February 2017

MAGARI 200 YA MSAFARA WA RAIS YATOWEKA GHANA…

Serikali mpya nchini Ghana inayatafuta magari 200 yaliyokuwa yakitumiwa na afisi ya rais ambayo yanadaiwa kutoweka, msemaji wa rais amesema.

Chama tawala kilihesabu magari hayo mwezi mmoja, kabla ya kuingia madarakani baada ya kupata ushindi uchaguzini mwezi Desemba mwaka jana.
Imekuwa kawaida kwa baadhi ya maafisa wa serikali inayoondoka kutorejesha magari ya serikali, na hulazimu serikali mpya kuyatwaa kwa nguvu nchini Ghama.
Waziri mmoja katika serikali iliyoondoka ya John Mahama, hata hivyo amesema kuenezwa kwa habari kwamba wenzake walitekeleza uhalifu ni makosa.
Aliyekuwa waziri wa usalama Omane Boamah amewaambia wana habari kuwa, hiyo ni mbinu inayotumiwa na serikali mpya kuipa sababu za kununua magari mapya.
Kituo cha redio cha Citi FM nchini Ghana kimeripoti kwamba rais amelazimika kutumia gari aina ya BMW lililoundwa miaka 10 iliyopita, kutokana na kutorejeshwa kwa magari hayo.

Alipokuwa anatoa taarifa yake Bw Arhin alifichua kwamba afisi ya rais ilifaa kuwa na magari zaidi ya 300 lakini hakueleza magari hayo hutumiwa vipi.

0 comments:

Post a Comment