Tuesday, 21 February 2017

MZEE AISHI CHINI YA MTI KWA MIAKA 15

Mzee wa miaka 72 ambaye alikuwa Ofisa Elimu Mkoa wa Tanga mwaka 1975, John Kihendo aliyestaafu mwaka 1989, ameamua kuishi chini ya mti kwa muda wa miaka 15 kwa madai kuwa anaitafuta haki ya shamba lake lenye ukubwa wa hekari sita lililoko kata ya Magomeni jijini Tanga.

Hivyo anaiomba serikali kumaliza mgogoro wa shamba hilo uliodumu kwa zaidi ya miaka saba ili aweze kapata haki yake na hatimaye ajenge makazi ya kudumu na familia yake.
Mzee alizungumza na kusema baada ya Wapimaji kuja eneo hilo walidai linatakiwa kutumika kama kituo cha jamii ‘(Community Centre)’  hivyo mwaka 2004 alipewa fidia kidogo ambayo haiendani na hilo eneo.
Ameeleza kuwa amekaa eneo hilo tangu mwaka 1978 ambapo  hivi sasa shamba lake limekuwa likivamiwa  na watu tofauti tofauti pasipo yeye kushirikishwa ikiwa  pamoja na kanisa kujengwa ndani ya shamba lake.
”Niliwahi kuchimba msingi katika hili shamba ili nijenge alikuja mwenyekiti wa mtaa na kuamuru ule msingi ufukiwe nisijenge hili eneo ni la kituo cha jamii (community centre)”.
Pia mzee huyo alisema ameshawahi kuandika barua kwa Mkurugenzi wa jiji kuwa sehemu yake ya shamba ambayo haijatathiminiwa kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1999 ya ardhi.

”Mimi ni mkulima wa shamba langu na sheria ile imeshapita kwa nini nisiipate ile sehemu yangu ambayo kwa miaka 7 haikutathiminiwa  kitu ambacho hakikutathiminiwa maana yake hakihitajiki basi ningepewa mimi mwenyewe nitumie ikiwemo kujenga nyumba yangu ya kudumu,” amesema mzee Kihendo.

Related Posts:

  • TUNDU LISSU ATEMA CHECHE…. Wakati Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu, akiwa bado anakabiliwa na kesi kadhaa za uchochezi, amefytuka tena na kutoa maneno mazito juu ya viongozi wa Serikali, huku akisema kwa … Read More
  • ROONEY AITEKA DAR………   Mshambuliaji mpya wa Everton Wayne Rooney, amekuwa kivutio wakati msafara wa timu hiyo ulipowasili jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Everton iliyowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa (JNIA) ilipokelewa na Wa… Read More
  • MUUGUZI AMDUNGA BINTI SINDANO NA KUMBAKA…… Muuguzi anayefanya kazi Kituo cha Afya Kata ya Igurubi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Damian Mgaya (26) anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma ya kumbaka binti wa miaka 18 mkazi wa kitongoji cha Mwagala B, Kijiji cha Mwagala.… Read More
  • WAUMINI WAWILI WAFA MAJI WAKIBATIZWA.. Waumini wawili wa Kanisa Siloam wamekufa maji wakibatizwa katika Mto Ungwasi wilayani Rombo baada ya mmoja wao kupandisha mapepo na kuwatumbukiza majini wenzake. Mkuu wa Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro Agnes Hokororo… Read More
  • WANAOTOA SIRI ZA SERIKALI MTANDAONI KUTUPWA JELA MIAKA 20.. Serikali imetoa onyo kwa watumishi wa umma wanaotoa siri za serikali na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii kuwa watachukuliwa hatua za kisheria. Onyo hilo lilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Waziri wa Ofisi ya R… Read More

0 comments:

Post a Comment