Tuesday 21 February 2017

MZEE AISHI CHINI YA MTI KWA MIAKA 15

Mzee wa miaka 72 ambaye alikuwa Ofisa Elimu Mkoa wa Tanga mwaka 1975, John Kihendo aliyestaafu mwaka 1989, ameamua kuishi chini ya mti kwa muda wa miaka 15 kwa madai kuwa anaitafuta haki ya shamba lake lenye ukubwa wa hekari sita lililoko kata ya Magomeni jijini Tanga.

Hivyo anaiomba serikali kumaliza mgogoro wa shamba hilo uliodumu kwa zaidi ya miaka saba ili aweze kapata haki yake na hatimaye ajenge makazi ya kudumu na familia yake.
Mzee alizungumza na kusema baada ya Wapimaji kuja eneo hilo walidai linatakiwa kutumika kama kituo cha jamii ‘(Community Centre)’  hivyo mwaka 2004 alipewa fidia kidogo ambayo haiendani na hilo eneo.
Ameeleza kuwa amekaa eneo hilo tangu mwaka 1978 ambapo  hivi sasa shamba lake limekuwa likivamiwa  na watu tofauti tofauti pasipo yeye kushirikishwa ikiwa  pamoja na kanisa kujengwa ndani ya shamba lake.
”Niliwahi kuchimba msingi katika hili shamba ili nijenge alikuja mwenyekiti wa mtaa na kuamuru ule msingi ufukiwe nisijenge hili eneo ni la kituo cha jamii (community centre)”.
Pia mzee huyo alisema ameshawahi kuandika barua kwa Mkurugenzi wa jiji kuwa sehemu yake ya shamba ambayo haijatathiminiwa kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1999 ya ardhi.

”Mimi ni mkulima wa shamba langu na sheria ile imeshapita kwa nini nisiipate ile sehemu yangu ambayo kwa miaka 7 haikutathiminiwa  kitu ambacho hakikutathiminiwa maana yake hakihitajiki basi ningepewa mimi mwenyewe nitumie ikiwemo kujenga nyumba yangu ya kudumu,” amesema mzee Kihendo.

0 comments:

Post a Comment