Friday, 17 February 2017

SIMU ZA NOKIA 3310 KUREJEA…?

Kuna taarifa kwamba huenda simu muundo wa Nokia 3310 zikazinduliwa upya na kuanza kuuzwa tena baadaye mwezi huu.

Kampuni ya HMD Global Oy ya Finland, ambayo ina haki za kuunda bidhaa za nembo ya Nokia ndiyo inayodaiwa kuwa na mipango hiyo.
Simu hizo inaarifiwa zitazinduliwa wakati wa Kongamano la Simu za Rununu Duniani baadaye mwezi huu.
Kampuni ya Nokia ilinunuliwa na Microsoft mwaka 2013.
Simu asilia za Nokia 3310 zilipata umaarufu kutokana na uthabiti wake.
Nokia 3310/3330, zilizinduliwa 2000, na ni miongoni mwa simu zilizouzwa sana duniani. Jumla ya simu 126 milioni za aina hiyo zilitengenezwa na Nokia.
Una kumbukumbu za simu hiyo?
Dave Mitchell nchini Uingereza anaamini kwamba anamiliki moja ya simu za zamani zaidi aina ya Nokia 3310 nchini Uingereza.
Alinunua simu hiyo mwaka 2000 na anasema amekuwa akiitumia tangu wakati huo - bila natatizo yoyote.
Mwanajeshi huyo wa zamani anasema simu hiyo imewahi kufuliwa pamoja na nguo kwenye mashine, ikakanyagwa na hata kutumbukia kwenye mchuzi.
Anasema huwa inamhitaji kuweka chaji baada ya siku kumi.

Bado ina betri yake asili.

Related Posts:

  • CHINA KUZINDUA MTANDAO USIODUKULIWA…. Wakati udukuzi wa mitandao wanapoendesha udukuzi zaidi, China inatarajiwa kuzindua mtandao usiodukuliwa ikimaanisha kuwa itakuwa rahis kugundua kabla ya wadukuzi kuingia. Mradi huo wa kichina katika mji wa Jinan na unau… Read More
  • BETRI KUBWA ZAIDI DUNIANI KUUNDWA.. Betri kubwa zaidi ya lithium duniani itaundwa na kuwekwa nchini Australia, kupitia makubaliano kati ya kampuni inayounda magari ya kutumia umeme ya Tesla na kampuni ya kawi ya Australia Neoen. Betri hiyo inatarajiwa kul… Read More
  • SAMSUNG YATUMIA SEHEMU ZA NOTE 7 KUUNDA SIMU MPYA….. Kampuni ya mawasiliano ya Samsung imeanza kuuza simu nyingine ambazo inasema imetumia baadhi ya sehemu na vipande vilivyokuwa kwenye simu za Galaxy Note 7 ambazo zilikumbwa na matatizo. Simu hizo za Galaxy Note 7 ziliku… Read More
  • UNAWEZA KUSAFIRI UKITUMIA NDEGE ISIYO NA RUBANI....? Hilo ndilo swali mamilioni ya watu huenda wakajiuliza siku za usoni ikiwa wanataka kusafiri kwenda likizo kote duniani. Tunaposogea karibu na kutumia magari yasiyokuwa na dereva, ambayo tayari yameingia barabarani katika… Read More
  • FACEBOOK KUJA NA RUNINGA YA MTANDAONI.. Kampuni kubwa zaidi ya mitandao ya kijamii duniani Facebook, inatarajia kuanza kutoa huduma ya video itakayokuwa ikiitwa ”watch” ama tazama. Facebook inasema kwamba imewekeza mamilioni ya dola katika kuufanya mfumo hu… Read More

0 comments:

Post a Comment