Thursday 16 February 2017

ZAIDI YA WATOTO 25,000 KUPATA KANSA KILA MWAKA..

Katika Kuadhimisha Siku ya Saratani duniani, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Asasi ya Marafiki wa Watoto wenye Saratani Tanzania (FoCC) Janeth Manoni, amesema kwa sasa ugonjwa huo umekuwa tishio kwa watoto nchini, ambapo inakadiriwa zaidi ya watoto 25,000 hupata ugonjwa huo kila mwaka.

Manoni ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema kuwa watoto wengi hufariki dunia baada ya kuchelewa kupata matibabu kufuatia jamii kutojua dalili za awali za ugonjwa huo..
Manoni amesema asasi yake itaadhimisha siku ya saratani Jumamosi ya Februari 18 katika viwanja vya Don Bosco, ambapo kutatolewa huduma za uchunguzi wa saratani kwa watoto bure, na kuwataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kufanyiwa uchunguzi.

Mhamasishaji wa FoCC Remigius Kazaura amesema kuwa, ongezeko la ugonjwa wa saratani kwa watoto linatokana na mabadiliko ya mfumo wa maisha hasa ulaji wa vyakula visivyo vya asili.

0 comments:

Post a Comment