Sunday, 5 February 2017

WHO: Saratani ilisababisha hasara ya dola trilioni 1.6 duniani mwaka 2010

Shirika la Afya Duniani, WHO limesema gharama za matibabu ya saratani ni kubwa kuliko zile za kinga na tiba wakati wa hatua za mwanzo za ugonjwa huo unaosababisha kifo cha mtu mmoja katika kila watu sita duniani kote.

WHO imetolea mfano mwaka 2010 ambapo gharama za kiuchumi na kiafya zilizotokana na saratani ilikuwa dola trilioni 1.16 duniani kote.
Ili kupunguza gharama, WHO imezindua mwongozo mpya wa kuwezesha nchi yoyote bila kujali kipato chake iweze kuimarisha ugunduzi wa saratani mapema.
WHO ilitoa kauli hiyo Jumamosi Februari Nne ambayo ni Siku ya Saratani Duniani. Kwa munasaba wa siku hiyo WHO imezindua mwongozo mpya wa kuwezesha uchunguzi wa mapema wa ugonjwa huo hatari unaosababisha vifo vya watu milioni 8.8 kila mwaka duniani, kati ya wagonjwa milioni 14 wanaobainika kuwa nao.
WHO inasema hali si shwari kwani idadi inaongezeka mwaka hadi mwaka na hivyo njia pekee ni kuimarisha mbinu za kubaini mapema kwani hata visababishi vya saratani navyo vinaongezeka.
Shirika hilo linasema saratani haipaswi kusalia adhabu ya kifo wakati huu ambapo kuna kampeni za kudhibiti visababishi kama vile matumizi ya tumbaku, unywaji wa pombe na mlo usio bora.

Related Posts:

  • UNYONYAJI KIDOLE UNAFAIDA KWA WATOTO- UTAFITI Ripoti mpya inasema watoto wanaonyonya vidole au kung'ata kucha zao kwa meno huenda wasipate matatizo ya kuathirika kutokana na mazingira hewa au kula vyakula fulani. Kwa mujibu wa waandishi katika jarida la Pedi… Read More
  • UNENE WA KUPITA KIASI……! Utafiti wa mmoja kiafya duniani umeonyesha ongezeko la asilimia 82 la watu wanene kupita kiasi kati ya mwaka wa 1990 na 2010, likasema jarida la tiba la Uingereza, ‘The Lancet’, Volume 387, la Aprili 2, 2016 Vifo v… Read More
  • MATIBABU YA KIFAFA CHA MIMBA….. Kifafa cha mimba ni ugonjwa unaowapata wanawake wajawazito, hasa wenye mimba za kwanza. Kwa walio wengi, ugonjwa huu hutokana na kupanda kwa msukumo wa damu (High blood pressure). Ugonjwa huu utokeapo, mgonjwa hupat… Read More
  • UTAFITI:UNENE UNAUA MAPEMA…!!   Utafiti wa kimataifa umegundua kuwa kunenepa kunahusiana moja kwa moja na visa vya watu kufa mapema, huku wanaume wakiwa katika uwezekano mara tatu wa kufariki zaidi ya wanawake. Kwa kutumia data kutoka takriban … Read More
  • HII NDIO NCHI INAYOONGOZA KWA WATU WAKE KUWA NA HIV..! Marekani imeiahidi Afrika Kusini msaada wa dola milioni 410, katika vita dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi. Afrika Kusini ina idadi kubwa zaidi ya watu wanaoishi na virusi vya HIV duniani. Msaada huo wa Marekani utasaidia kati… Read More

0 comments:

Post a Comment