Friday, 10 February 2017

MKALIMANI FEKI WA MTALII ATIWA NGUVUNI

Mwongoza Watalii (Guide), ambaye anadaiwa kupotosha tafsiri ya matamshi ya mtalii aliyekuwa amemaliza kutembelea Mamlaka ya Bonde la Ngorongoro (NCAA), ametiwa mbaroni.
Video ya mwongoza watalii huyo, ilianza kusambaa katika mitandao ya kijamii wiki iliyopita, na kuzua taharuki katika sekta ya Utalii nchini,huku wadau wengi wakitaka asakwe na kukamatwa.
Katika video hiyo, mtalii huyo ambaye jina lake halikupatikana mara moja, anaonekana akisema safari yake nchini Tanzania imekuwa nzuri na watanzania aliokutana nao walikuwa ni watu wenye upendo.
Akizungumza na gazeti hili kwa simu leo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, alisema mara baada ya kuona video hiyo kwenye mitandao aliagiza akamatwe mara moja.

“Nilitoa maagizo jana (juzi) usiku atafutwe na akamatwe na taarifa nilizopewa leo ni kuwa ameshakamatwa kwenye gate (lango) la Nabi Serengeti na yuko rumande kule Mugumu”alisema.

Related Posts:

  • MBOWE NA MDEE WASEMA WALICHOHOJIWA KWA SAA MBILI. Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), jana wamehojiwa na Kamati ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge kwa muda wa saa mbili – saa moja kila mmoja. Wamehojiwa na kam… Read More
  • MBARONI AKIPENYEZA SIMU TANO GEREZA LA KEKO DAR… Ramadhani Nombo anashikiliwa na Jeshi la Polisi kituo cha Chang’ombe Temeke jijini Dar es Salaam, kwa kosa la kupenyeza simu tano kwenye gereza la Keko. Mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya chakula alichopeleka gerezani, … Read More
  • HAJI MANARA ATOA POLE KWA RAIS TFF….. Mara baada ya taarifa kutoka Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) kuwashikilia Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania  (TFF), Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wake Mwesigwa Celestine, kwa tuhuma za… Read More
  • MBARONI KWA KWA UBAKAJI… Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia Samweli Masumbuko (32), Mkazi wa Kata ya Mahina wilayani Nyamagana, kwa tuhuma za kumbaka  mwanafunzi wa darasa la pili (jina linahifadhiwa) mwenye umri wa miaka 10. Kwa… Read More
  • BENKI YA FBME YAFUNGWA KWA MADAI YA UTAKATISHAJI WA FEDHA HARAMU…… Benki kuu ya Tanzania inasema kuwa imeipokonya leseni ya kuhudumu benki ya FBME ya Tanzania baada ya kushutumiwa na serikali ya Marekani kwa utakatishaji wa fedha haramu, kulingana na chombo cha habari cha Reuters. Benk… Read More

0 comments:

Post a Comment