Tuesday, 14 February 2017

MAHARUSI WALIOTUMIA DOLA PEKEE WAANDALIWA HARUSI YA KIFAHARI KENYA

Maharusi waliowasisimua wengi baada ya kutumia Sh100 pekee za Kenya kugharimia harusi, wameandaliwa sherehe ya harusi ya kufana jijini Nairobi.

Sherehe hiyo ya marudio imeandaliwa katika bustani ya Eden Bliss, Nairobi ulimwengu ukiandhimisha Siku ya Wapendanao.
Harusi ya Anne na Wilson Mutura ya awali iligharimu dola moja pekee ya Kimarekani lakini sherehe ya sasa imegharimu takriban Sh3.5 milioni (Dola 35,000).
Pesa hizo zimegharimiwa na makundi mbalimbali yanayohusika katika uandaaji wa sherehe, ambayo yaliungana kwa pamoja na kuchanga pesa kuandalia Anne na Wilson sherehe ya kukata na shoka.
Wawili hao wanaoishi eneo la Kasarani Nairobi, walisifiwa kwa kuonyesha thamani halisi ya mapenzi badala ya kuongozwa na pesa.
Kando na kuandaliwa harusi hiyo, wametunukiwa shamba la kilimo cha kisasa, fungate kwenye hoteli ya kifahari na baada ya sherehe ya leo wanatarajiwa kwenda kwa fungate nyingine mjini Dubai.
Dola yenyewe walioyotumia Anne na Wilson katika harusi yao waliitumia kununua pete mbili.
Walikuwa wameahirisha harusi yao mara tatu baada ya kukosa fedha za kutosha kuandaa sherehe kubwa ya harusi.
Maombi yao kwa familia na marafiki kuwafanyia mchango, hayakutimizwa.
Baada ya muda Bwana harusi Wilson, hakuwa na la kufanya ila kumshawishi mpenzi wake kuhusu uwezo wake.


Related Posts:

  • VIONGOZI WA MADAKTARI KENYA WAFUNGWA JELA.. Mahakama ya masuala ya wafanyakazi nchini Kenya, imewahukumu viongozi saba wa chama cha wahudumu wa afya (KMPDU) kufungwa jela mwezi mmoja. Hatua hiyo inafuatia Viongozi hao kukaidi agizo la kumaliza mgomo ambao umedumu… Read More
  • PLAYBOY KUCHAPISHA TENA PICHA ZA UTUPU.. Jarida la Playboy limetangaza kwamba litaanza kuchapisha tena picha za utupu, na kubatilisha uamuzi wa awali uliotolewa mwishoni mwa mwaka jana. Hatua ya sasa imetangazwa na afisa mkuu mpya wa ubunifu katika jarida hilo … Read More
  • MAHARUSI WALIOTUMIA DOLA PEKEE WAANDALIWA HARUSI YA KIFAHARI KENYA Maharusi waliowasisimua wengi baada ya kutumia Sh100 pekee za Kenya kugharimia harusi, wameandaliwa sherehe ya harusi ya kufana jijini Nairobi. Sherehe hiyo ya marudio imeandaliwa katika bustani ya Eden Bliss, Nairobi u… Read More
  • AMUUA MFANYAKAZI AKIDHANI NI NGIRI AFRIKA KUSINI.. Watu nchini Afrika Kusini wamegadhabishwa, kufuatia taarifa za mwanamme mmoja, ambaye analaumiwa kwa kumuua kwa kumpiga risasi mfanyakazi wa shamba, akidhani kuwa mtu huyo ni ngiri. Stephen Hepburn alifikishwa mahakaman… Read More
  • KWA UDANGANYIFU KWENYE MITIHANI.. Mahakama ya Juu nchini India imefuta leseni za madaktari 634 ambao wamejipata kwenye sakata ya wanafunzi kutumia udanganyifu kujiunga na vyuo vya mafunzo ya udaktari katika jimbo la Madhya Pradesh. Mamia ya wanafunzi,… Read More

0 comments:

Post a Comment