Thursday 2 February 2017

KIONGOZI WA UPINZANI DRC AFARIKI DUNIA.

Kiongozi wa upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Etienne Tshisekedi, amefariki dunia mjini Brussels nchini Ubelgiji akiwa na umri wa miaka 84.

Tshisekedi alikwenda mjini Brussels mwishoni mwa mwezi january kwa ajili ya matibabu.
Bwana Tshisekedi alikuwa mmoja wa wanasiasa wakongwe waliokuwa mstari wa mbele kupigania demokrasia ya nchi yake.
Alisimama kidete katika utawala wa aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo Rais Mobutu Sese Seko, ambae utawala wake ulidumu kwa miongo kadhaa kabla ya kupinduliwa.

Etienne Tshisekedi pia alikuwa mpinzani wa Rais Laurent Kabila, ambae aliingia madarakani mnamo mwaka 1997, na mwanae Rais Joseph Kabila ambae hivi sasa ndio anatawala nchi hiyo.

0 comments:

Post a Comment