Thursday, 9 February 2017

BUNGE LAWAITA MAKONDA, MNYETI KUJIELEA..

Bunge limepitisha kwa kauli moja, azimio la kuitwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul  Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti ili kuhojiwa na Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge.

Azimio hilo limetokana na hoja iliyowasilishwa na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara akisema wateule hao wa Rais wametoa kauli zinazodhalilisha hadhi ya mhimili huo wa Dola.
Akijibu swali kuhusu tuhuma dhidi yake zilizoibuliwa na wabunge kuhusu chanzo cha mali zake, Makonda amewaambia waandishi wa habari kuwa wakati mwingine watunga sheria hao hulala bungeni kwa kukosa cha kuzungumza.
Aidha, kutokana na wabunge kukerwa na kauli ya Makonda, mbunge wa Mkuranga (CCM), Abdallah Ulega ameomba mwongozo kuhusu suala hilo.

Hata hivyo, Mkuu wa wilaya, Mnyeti anadaiwa kuandika kwenye ukurasa wake wa Facebook kuwa wabunge ni wapuuzi kutokana na michango yao wakati walipohoji hatua ya Ma-DC na Ma-RC kutoa amri za kuwaweka mahabusu viongozi wa kisiasa

Related Posts:

  • HAJI MANARA ATOA POLE KWA RAIS TFF….. Mara baada ya taarifa kutoka Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) kuwashikilia Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania  (TFF), Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wake Mwesigwa Celestine, kwa tuhuma za… Read More
  • MAITI TATU 3 ZAOKOTOWA KWENYE VIROBA... Maiti tatu zimeokotwa kwenye fukwe mbalimbali za Zanzibar katika siku tatu zilizopita zikiwa zimeharibika vibaya, kuwa na majeraha ya kukatwa na kitu chenye makali zikiwa zimefungwa kwenye viroba Maiti ya mwisho iliokot… Read More
  • MBARONI AKIPENYEZA SIMU TANO GEREZA LA KEKO DAR… Ramadhani Nombo anashikiliwa na Jeshi la Polisi kituo cha Chang’ombe Temeke jijini Dar es Salaam, kwa kosa la kupenyeza simu tano kwenye gereza la Keko. Mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya chakula alichopeleka gerezani, … Read More
  • MBUNGE KIBITI ASEMA ANAMUACHIA MUNGU........ Matukio ya kihalifu na mauaji yanayofanywa na watu wasiofahamika, yameendelea kutokea wilayani Kibiti baada ya viongozi wawili wa Kijiji cha Mangwi, Kata ya Mchukwi kuuawa kwa kupigwa kwa risasi, huku Mbunge wa Jimbo la K… Read More
  • DPP ASUBIRI FAILI LA LOWASSA………. Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Biswalo Mganga, amesema anasubiri Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) imalize uchunguzi wake dhidi ya tuhuma zinazomkabili Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa. Lowa… Read More

0 comments:

Post a Comment