Thursday, 9 February 2017

UBER KUTENGEZA MAGARI YANAYORUKA..

Muhandisi wa zamani wa shirika la maswala ya angani Nasa ameajiriwa na kampuni ya teksi Uber kusaidia katika utafiti wake wa kutengeza magari yanayoruka.

Mark Moore anajiunga na Uber kama mkurugenzi wa uhandisi wa angani.
Lengo la Uber katika kutengeza magari yanayoruka liliangaziwa mwezi Oktoba ambapo maswala ya kupaa na kutua yalijadiliwa.
Uber tayari inawekeza katika magari ya kujiendesha ikishirikiana na kampuni ya Volvo na Daimler.
Katika mipango yake Uber imesema kuwa katika mahitaji ya angani ,kampuni hiyo ina uwezo wa kuimarisha uchukuzi wa mijini na kuwapatia wateja wake muda wanaopoteza kila siku wanaposafiri.

''Huku majumba marefu yakisaidia katika utumizi mchache wa ardhi, uchukuzi wa mijini utatumia maneeo matatu ya angani kukabiliana na msongamano wa magari ardhini''.
Mpango huo utashirikisha mtandao wa ndege za kielektroniki ambazo zitapaa na kushuka wima.
Moore alifichua mpango kama huo katika jarida lililochapishwa wakati alipokuwa Nasa.
Alisema kuwa mpango wa kutengeza vitu vinavyopaa kielektroniki ni mpango muhimu wa kiteknolojia wa ndege na kuongezea kwamba kitu kinachozuia kuanza kwa mpango huo ni betri zitakazotumika.

Kampuni ya kutengeza magari ya ya Aeromobil kutoka nchini Slovakia ni miongoni mwa kampuni ambazo zina mpango wa kutengeza gari la kuruka ambayo inatarajiwa kuingia katika soko mwaka huu.

Related Posts:

  • UBER KUTENGEZA MAGARI YANAYORUKA.. Muhandisi wa zamani wa shirika la maswala ya angani Nasa ameajiriwa na kampuni ya teksi Uber kusaidia katika utafiti wake wa kutengeza magari yanayoruka. Mark Moore anajiunga na Uber kama mkurugenzi wa uhandisi wa angan… Read More
  • INDIA YAWEKA REKODI KWA KURUSHA SATELAITI 104… India imeweka rekodi mpya kwa kuwa taifa lililorusha setilaiti nyingi angani kwa wakati mmoja baada ya kurusha setilaiti 104 kwa pamoja. Rekodi ya awali iliwekwa na Urusi mwaka 2014, ambayo ilikuwa setilaiti 37. Kati… Read More
  • SIMU ZA NOKIA 3310 KUREJEA…? Kuna taarifa kwamba huenda simu muundo wa Nokia 3310 zikazinduliwa upya na kuanza kuuzwa tena baadaye mwezi huu. Kampuni ya HMD Global Oy ya Finland, ambayo ina haki za kuunda bidhaa za nembo ya Nokia ndiyo inayodaiwa k… Read More
  • SAMSUNG YATUMIA SEHEMU ZA NOTE 7 KUUNDA SIMU MPYA….. Kampuni ya mawasiliano ya Samsung imeanza kuuza simu nyingine ambazo inasema imetumia baadhi ya sehemu na vipande vilivyokuwa kwenye simu za Galaxy Note 7 ambazo zilikumbwa na matatizo. Simu hizo za Galaxy Note 7 ziliku… Read More
  • TCRA YATOA ONYO KUHUSU VIRUSI MTANDAONI… Kufuatia tishio la kuwapo programu mtumishi (software) yenye virusi aina ya WannaCry, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa onyo kwa watumiaji wa kompyuta kutofungua viambatanishi wasivyovijua kwenye barua pepe za… Read More

0 comments:

Post a Comment