Monday 13 February 2017

VIONGOZI WA MADAKTARI KENYA WAFUNGWA JELA..

Mahakama ya masuala ya wafanyakazi nchini Kenya, imewahukumu viongozi saba wa chama cha wahudumu wa afya (KMPDU) kufungwa jela mwezi mmoja.

Hatua hiyo inafuatia Viongozi hao kukaidi agizo la kumaliza mgomo ambao umedumu kwa zaidi ya miezi miwili.
Jaji Hellen Wasilwa amesema viongozi hao hawajatoa sababu ya kutosha kuonesha ni kwa nini hawajamaliza mgomo huo.
Ameamuru mazungumzo ya kumaliza mgomo huo yaendelee.
Jaji Wasilwa alikuwa awali amewapa viongozi hao muda wa wiki mbili kumaliza mgomo huo, na baadaye akawaongezea siku tano.
Mazungumzo ya kumaliza mgomo huo hata hivyo hayakuzaa matunda kipindi hicho.
Madaktari wamekuwa wakiitaka serikali kuheshimu makubaliano ya mwaka 2013, ya kuwaongezea mishahara.
Wamekataa mshahara walioongezewa na serikali wa asilimia 40 wakisema kuwa ni wa chini kuliko ule walioafikiana mwaka 2013.


0 comments:

Post a Comment