Monday, 13 February 2017

VIONGOZI WA MADAKTARI KENYA WAFUNGWA JELA..

Mahakama ya masuala ya wafanyakazi nchini Kenya, imewahukumu viongozi saba wa chama cha wahudumu wa afya (KMPDU) kufungwa jela mwezi mmoja.

Hatua hiyo inafuatia Viongozi hao kukaidi agizo la kumaliza mgomo ambao umedumu kwa zaidi ya miezi miwili.
Jaji Hellen Wasilwa amesema viongozi hao hawajatoa sababu ya kutosha kuonesha ni kwa nini hawajamaliza mgomo huo.
Ameamuru mazungumzo ya kumaliza mgomo huo yaendelee.
Jaji Wasilwa alikuwa awali amewapa viongozi hao muda wa wiki mbili kumaliza mgomo huo, na baadaye akawaongezea siku tano.
Mazungumzo ya kumaliza mgomo huo hata hivyo hayakuzaa matunda kipindi hicho.
Madaktari wamekuwa wakiitaka serikali kuheshimu makubaliano ya mwaka 2013, ya kuwaongezea mishahara.
Wamekataa mshahara walioongezewa na serikali wa asilimia 40 wakisema kuwa ni wa chini kuliko ule walioafikiana mwaka 2013.


Related Posts:

  • MAGARI 200 YA MSAFARA WA RAIS YATOWEKA GHANA… Serikali mpya nchini Ghana inayatafuta magari 200 yaliyokuwa yakitumiwa na afisi ya rais ambayo yanadaiwa kutoweka, msemaji wa rais amesema. Chama tawala kilihesabu magari hayo mwezi mmoja, kabla ya kuingia madarakani… Read More
  • PLAYBOY KUCHAPISHA TENA PICHA ZA UTUPU.. Jarida la Playboy limetangaza kwamba litaanza kuchapisha tena picha za utupu, na kubatilisha uamuzi wa awali uliotolewa mwishoni mwa mwaka jana. Hatua ya sasa imetangazwa na afisa mkuu mpya wa ubunifu katika jarida hilo … Read More
  • VIONGOZI WA MADAKTARI KENYA WAFUNGWA JELA.. Mahakama ya masuala ya wafanyakazi nchini Kenya, imewahukumu viongozi saba wa chama cha wahudumu wa afya (KMPDU) kufungwa jela mwezi mmoja. Hatua hiyo inafuatia Viongozi hao kukaidi agizo la kumaliza mgomo ambao umedumu… Read More
  • MAHARUSI WALIOTUMIA DOLA PEKEE WAANDALIWA HARUSI YA KIFAHARI KENYA Maharusi waliowasisimua wengi baada ya kutumia Sh100 pekee za Kenya kugharimia harusi, wameandaliwa sherehe ya harusi ya kufana jijini Nairobi. Sherehe hiyo ya marudio imeandaliwa katika bustani ya Eden Bliss, Nairobi u… Read More
  • KWA UDANGANYIFU KWENYE MITIHANI.. Mahakama ya Juu nchini India imefuta leseni za madaktari 634 ambao wamejipata kwenye sakata ya wanafunzi kutumia udanganyifu kujiunga na vyuo vya mafunzo ya udaktari katika jimbo la Madhya Pradesh. Mamia ya wanafunzi,… Read More

0 comments:

Post a Comment