Thursday, 2 February 2017

MAJALIWA: RAIS HAJATANGAZA KUFUTA VYAMA VYA UPINZANI

 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Rais Dkt. John Magufuli hajawahi kutangaza ama kutoa kauli ya kufutwa kwa vyama vya siasa nchini.

Ameyasema hayo leo Bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe  katika kipindi cha maswali na majibu kwa Waziri Mkuu.
Mbowe amesema Rais Dkt. Magufuli alinukuliwa akisema atahakikisha anafuta vyama vya upinzani ifikapo mwaka 2020 ata hakikisha hakuna upinzani nchini, pia alitaka kujua nini kauli ya Serikali kuhusu kunyimwa dhamana kwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ambaye anashikiliwa kwa muda miezi mitatu.
Aidha, wakati akijibu swali hilo Waziri Mkuu amesema kuwa Rais Dkt. John Magufuli hajawahi kutangaza kufutwa kwa vyama vya siasa ifikapo 2020.
“Kwanza nataka nikanushe kwamba Mheshimiwa Rais hajawahi kutangaza kuvifuta vyama vya upinzani. Pia Watanzania wote wanajua nchi hii inaongozwa kwa sheria, kanuni na taratibu,” amesema Waziri Mkuu.
Amesema kuwa wanaongoza nchi kwa kufuata mihimili mitatu ambayo ni Serikali, Mahakama na Bunge na kwamba hakuna mhimili unaoweza kuingilia mwingine.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amewahakikishia Watanzania kwamba suala la upungufu wa sukari halitatokea nchini kwa sababu viwanda vya ndani vinaendelea kuzalisha na hadi mwishoni mwa Januari vilifikia asilimia 86 ya uzalishaji.

Related Posts:

  • MWENYEKITI WA CCM MBEYA ANUSURIKA KUUAWA.. Mwenyekiti wa CCM Mbeya Mjini, Efrahim Mwaitenda mwenye umri wa miaka 60 amejeruhiwa kwa kupigwa risasi mgongoni na mtu au watu wasiofahamika. Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Emmanuel Lukula amesema tukio hilo li… Read More
  • ANASWA NA MAHINDI YA BEI CHEE KUTOKA NJE YA NCHI Mfanyabiashara aliyejulikana kwa jina moja la JAPHET amekamatwa na kikosi maalum  kinachohusisha TRA , POLISI na MAAFISA WA KILIMO akiwa anavusha mahidi kwa njia ya panya kutoka nchini Malawi bila ya kufuata u… Read More
  • AHUKUMIWA KIFUNGO KWA KULALA NA MPENZI WA MWANAE… Mwanamke mmoja ambaye ametambulika kwa jina la Alaine Goodman (46) amehukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani baada ya kukutwa na hatia ya kufanya mapenzi na kijana mwenye umri mdogo ambaye ni mpenzi wa mtoto wake. G… Read More
  • HAKIMU MMOJA ASIKILIZA MASHAURI 400 KWA MWEZI.... Imeelezwa kuwa uhaba wa mahakimu katika Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi imefanya kila hakimu katika mahakama hiyo kuwa na mzigo wa mashauri 400 kwa mwezi mmoja. kufuatia hali hiyo, mahakama imeomba Mabaraza za Ardhi ya V… Read More
  • SUDAN YAPINGA AMRI YA TRUMP..! Wizara ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Sudan imemuita mwanabalozi wa Marekani mjini Khartoum kupinga hatua ya Rais Donald Trump ya kuwapiga marufuku raia wa nchi hiyo kuingia Marekani. Sudan inasema kuwa hatua hiyo… Read More

0 comments:

Post a Comment