Wednesday, 1 February 2017

FAHAMU MADHARA YA MATUMIZI YASIYO SAHIHI YA ANTIBIOTICS…

Vijisumu (antibiotics) ni mojawapo ya dawa muhimu zinazotumika mara kwa mara katika kutibu magonjwa mbalimbali yatokanayo na vimelea.


Dawa hizi hutibu magonjwa kwa ama kuua bacteria au kupunguza uwezo wake wa kuzaliana. Ingawaje vijisumu ni muhimu katika matibabu ya magonjwa mbali mbali kama zikitumiwa ipasavyo, lakini matumizi mabaya huleta madhara kwa mtumiaji.
Mfano wa dawa hizi ni ampicillin, ciprofloxacin, tetracycline, gentamycin, Pen V, erythromycin, metronidazole, Amoxillin.
Moja ya changamoto kubwa katika matibabu ni pale baadhi ya bacteria wanapojenga usugu dhidi ya dawa hizi. Kijiuasumu kikitumiwa kwa mda mrefu baadhi ya bacteria hujenga usugu ya dawa hizo hivyo na hivyo kutokuwawa na kijisuasumu hicho, hii ndiyo inayojulikana kama usugu dhidi ya vijiuasumu. Kwa sasa magonjwa yanayosababishwa na bacteria ambao ni sugu kwa baadhi ya vijiuasumu.
Ugonjwa unaotokana na bacteria hawa unakuwa mgumu kutibika na unaweza kuambukizwa kwa watu wengine. Ili kutibu ugonjwa unaotokana na bacteria hawa sugu unahitaji dawa yenye nguvu zaidi na uangalizi wa hali ya juu.
Kutumia vijiuasumu kiholela huweza kusababisha usugu wa bacteria na hivyo kushindwa kufanya kazi ipasavyo. Matumizi mabaya ya vijiua sumu ni mojawapo ya sababu zinazoleta usugu huo. Epuka matumizi yasiyosahihi ya vijiuasumu.
Mifano ya matumizi yasiyosahihi ya vijiua sumu:
• Kutotumia dozi kamili ya vijiuasumu na kwa muda uliolekezwa.
• Kutumia vijiuasumu kutibu magonjwa yasiyohitaji vijiuasumu kwa mfano ugonjwa kama mafua ambao husababishwa na virusi au aleji.
• Kutumia dawa zinazokinzana kiutendaji kwa pamoja, kwa mfano baadhi ya vijiuasumu na vidonge vya uzazi wa mpango.
• Kunywa pombe wakati ukiwa kwenye dozi ya dawa ambapo ulishauliwa usinywe pombe.
• Kununua kiholela na kutumia dawa bila kufanyiwa uchunguzi.
• Kutumia dozi isiyo sahihi.
Ili kuepuka au kupunguza kutokea na usugu wa bacteria unashauriwa kutumia dawa zako kwa usahihi:

• Usinunue vijisumu bila cheti cha daktari.
• Usinunue kijisumu kiholela.
• Usitumie cheti cha dawa alichoandikiwa mtu mwingine.
• Usimpe mgonjwa mwingine dawa zako.
• Usikatishe dozi unapojisikia nafuu.
• Hakikisha unafahamu matumizi sahihi ya dawa ulizopewa kabla ya kurudi nyumbani.
• Tumia dozi sahihi kipindi chote cha matibabu.

Related Posts:

  • VYOMBO VYA PLASTIKI CHANZO CHA SARATANI…. Imebainika kuwa vifaa vya plastiki hutengenezwa kwa kemikali zaidi ya 200, hivyo kuwa chanzo cha aina 100 za ugonjwa wa saratani. Vifaa hivyo vya plastiki ni pamoja na mifuko ya rambo, bakuli, vikombe na vifaa vya kuhif… Read More
  • ZAIDI YA WATOTO 25,000 KUPATA KANSA KILA MWAKA.. Katika Kuadhimisha Siku ya Saratani duniani, Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Asasi ya Marafiki wa Watoto wenye Saratani Tanzania (FoCC) Janeth Manoni, amesema kwa sasa ugonjwa huo umekuwa tishio kwa watoto nchini, ambapo in… Read More
  • JE, WAJUA KUWA USINGIZI HUSABABISHA UGONJWA WA KUNENEPA..? Kulala kwa masaa mengi au kwa muda mfupi vinaweza kuchangia mtu kunenepa kupita kiasi Utafiti umegundua kuwa usingizi usio mzuri unaweka mtu kwenye hatari ya kunenepa kupita kiasi kwa watu walio na maumbile ya kunenep… Read More
  • WAGONJWA SASA KUWEKEWA MOYO BANDIA... Nchini Marekani kila baada ya dakika 10 mtu mmoja huwekwa kwenye foleni ya watu wanaosubiri kuwekewa moyo mpya ili kuweza kuendelea kuishi. Hali hii hutokea baada ya moyo wa mgonjwa kuonekana hauwezi kufanyiwa matibabu … Read More
  • NYANYA NDIO TUNDA NI MAARUFU ZAIDI DUNIANI..! Ikiwa ungeulizwa kutaja tunda bora zaid duniani, labda nyanya haitakuwa akilini mwako. Lakini unalolihitaji kulifahamu ni kuwa nyanya huzalishwa kwa wingi zaidi duniani kuliko tunda lolote lile. Baadhi ya watu hudai ku… Read More

0 comments:

Post a Comment