Saturday 18 February 2017

SIMU YA ADOLF HITLER KUPIGWA MNADA MAREKANI.

Simu iliokuwa ikitumiwa na kiongozi wa Wanazi Adolf Hitler kupigwa mnada Marekan
Simu iliyokuwa ikitumiwa na Adolf Hitler wakati wa vita vikuu vya pili vya Dunia itapigwa mnada nchini Marekani mwisho mwa juma hili.
Simu hiyo nyekundu iliyo na chapa cha jina la kiongozi huyo wa Wanazi, ilipatikana katika ngome ya Hitler jijini Berlin mwaka 1945.
Wanajeshi wa Urusi walimpa mwanajeshi wa Uingereza, Brigedia Sir Ralph Rayner, kama kito cha kumbukumbu, muda mfupi baada ya Ujerumani kukubali kushindwa katika vita hivyo.
Kampuni hiyo ya mnada iliyoko Maryland, ilisema kuwa shughuli za mnada zitaanza kwa bei ya Dola 100,000.

0 comments:

Post a Comment