Wednesday 15 February 2017

INDIA YAWEKA REKODI KWA KURUSHA SATELAITI 104…

India imeweka rekodi mpya kwa kuwa taifa lililorusha setilaiti nyingi angani kwa wakati mmoja baada ya kurusha setilaiti 104 kwa pamoja.

Rekodi ya awali iliwekwa na Urusi mwaka 2014, ambayo ilikuwa setilaiti 37.
Kati ya setilaiti hizo zilizorushwa India, ni tatu pekee ambazo ni za taifa hilo huku nyingi ziiwa ni za Marekani.
Setilaiti hizo zilirushwa kutoka kituo cha safari za anga za juu cha Sriharikota katika eneo la Andhra Pradesh mashariki mwa India.
Wachanganuzi wanasema ufanisi huo ni ishara kwamba, India imeanza kuibuka kuwa mhusika mkuu katika sekta ya safari za anga za juu yenye thamani ya mabilioni ya dola.
Kati ya setilaiti 104 zilizorushwa kutoka India, 96 ni za Marekani na hizo nyingine ni za kutoka mataifa mengine yakiwemo Israel, Kazakhstan, Umoja wa Milki za Kiarabu, Uswizi na Uholanzi.
Setilaiti ya ramani ya India ambao inaaminika kuwa na uwezo wa kupicha picha za ubora wa hali ya juu sana kutoka angani, ni miongoni mwa setilaiti zilizorushwa angani.
Setilaiti hiyo inatarajiwa kutumiwa na India kufuatilia shughuli za washindani wake katika bara la Asia, Pakistan na China.
Serikali ya India iliongeza bajeti yake kwa mpango wake wa anga za juu mwaka huu, na pia ikatangaza mpango wa kutuma chombo sayari ya Zuhura (Venus).

0 comments:

Post a Comment