Wednesday, 15 February 2017

INDIA YAWEKA REKODI KWA KURUSHA SATELAITI 104…

India imeweka rekodi mpya kwa kuwa taifa lililorusha setilaiti nyingi angani kwa wakati mmoja baada ya kurusha setilaiti 104 kwa pamoja.

Rekodi ya awali iliwekwa na Urusi mwaka 2014, ambayo ilikuwa setilaiti 37.
Kati ya setilaiti hizo zilizorushwa India, ni tatu pekee ambazo ni za taifa hilo huku nyingi ziiwa ni za Marekani.
Setilaiti hizo zilirushwa kutoka kituo cha safari za anga za juu cha Sriharikota katika eneo la Andhra Pradesh mashariki mwa India.
Wachanganuzi wanasema ufanisi huo ni ishara kwamba, India imeanza kuibuka kuwa mhusika mkuu katika sekta ya safari za anga za juu yenye thamani ya mabilioni ya dola.
Kati ya setilaiti 104 zilizorushwa kutoka India, 96 ni za Marekani na hizo nyingine ni za kutoka mataifa mengine yakiwemo Israel, Kazakhstan, Umoja wa Milki za Kiarabu, Uswizi na Uholanzi.
Setilaiti ya ramani ya India ambao inaaminika kuwa na uwezo wa kupicha picha za ubora wa hali ya juu sana kutoka angani, ni miongoni mwa setilaiti zilizorushwa angani.
Setilaiti hiyo inatarajiwa kutumiwa na India kufuatilia shughuli za washindani wake katika bara la Asia, Pakistan na China.
Serikali ya India iliongeza bajeti yake kwa mpango wake wa anga za juu mwaka huu, na pia ikatangaza mpango wa kutuma chombo sayari ya Zuhura (Venus).

Related Posts:

  • UNAWEZA KUSAFIRI UKITUMIA NDEGE ISIYO NA RUBANI....? Hilo ndilo swali mamilioni ya watu huenda wakajiuliza siku za usoni ikiwa wanataka kusafiri kwenda likizo kote duniani. Tunaposogea karibu na kutumia magari yasiyokuwa na dereva, ambayo tayari yameingia barabarani katika… Read More
  • CHINA KUZINDUA MTANDAO USIODUKULIWA…. Wakati udukuzi wa mitandao wanapoendesha udukuzi zaidi, China inatarajiwa kuzindua mtandao usiodukuliwa ikimaanisha kuwa itakuwa rahis kugundua kabla ya wadukuzi kuingia. Mradi huo wa kichina katika mji wa Jinan na unau… Read More
  • SAMSUNG WAZINDUA TOLEO JIPYA LA GALAXY… Kampuni ya simu za mkononi ya Sumsung, imezindua simu yake mpya ya Galaxy Note 8, ambayo ni ya kisasa zaidi na yenye ushindaji zaidi katika soko. Hatua hii inakuja baada ya kampuni hii kupata msukosuko wa kibiashara i… Read More
  • HUYU NI MTU ANAYEFUNZA KOMPYUTA KUTAMBUA HARUFU… Raia wa Nigeria Oshi Agabi amezindua kompyuta zinazotumia neva za panya katika kongamano la kiteknolojia la TEDGlobal linaloendelea nchini Tanzania. Mfumo huo umefunzwa kutambua harufu ya vilipuzi na unaweza kutumiwa ka… Read More
  • FACEBOOK KUJA NA RUNINGA YA MTANDAONI.. Kampuni kubwa zaidi ya mitandao ya kijamii duniani Facebook, inatarajia kuanza kutoa huduma ya video itakayokuwa ikiitwa ”watch” ama tazama. Facebook inasema kwamba imewekeza mamilioni ya dola katika kuufanya mfumo hu… Read More

0 comments:

Post a Comment