Thursday, 2 February 2017

MWALIMU ADAIWA KUSABABISHA KIFO CHA MWANAFUNZI KENYA.

Polisi nchini Kenya inachunguza kifo cha mwanafunzi wa darasa la tatu ambaye anadaiwa kupoteza maisha kufuatia kupigwa fimbo na mwalimu wake ambazo zilimsababishia majeruhi mwili mwake.

Akizungumza kuhusu tukio hilo Mkuu wa Polisi wa Kieni, Michael Mbaluku alimtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Joy Wangare (10) ambaye ni mwanafunzi wa Shuleya Msingi Macadamia.
Mbaluku alisema kuwa kabla ya kufariki mwanafunzi huyo, bibi wa marehemu alifungua kesi ya shambulizi Polisi na siku chache baada ya majeruhi kupatiwa matibabu alipoteza maisha hali ambayo ilizua taharuki kwa familia ya marehemu wakiamini kuwa fimbo alizochapwa mtoto wao ndiyo chanzo cha kifo.
“Bibi wa binti huyo alikuja kuripoti kesi ya shambulio dhidi ya mwalimu na tulimpa kibali ampeleke akapatiwe matibabu. Taarifa ambayo tulipokea siku chache kabla hajafariki alikwenda katika Hospitali ya Mary Immaculate na kupatiwa matibabu,” alisema Mbaluku na kuongeza.

“Hatuwezi kumshikilia muuaji kwasasa sababu ya mazingira ya kifo jinsi yalivyo tunasubiri taratibu za kisheria zikamilike, tumewataka wawe na subira na wasubiri matokeo ya uchunguzi, ikiwa ni pamoja na ripoti ya uchunguzi wa marehemu.”

Related Posts:

  • MSUSI MWENYE UMRI WA MIAKA 93 ASTAAFU... Msusi mmoja amestaafu baada ya kufanya kazi kwenye duka moja la urembo kwa miaka jumla ya 72. Kathleen Privett mwenye umri wa miaka 93, ameamua kufunga duka hilo lililo Drayton, Portsmouh, ambalo lilianzishwa na babaka … Read More
  • MWANAMUME ATAMIA MAYAI YA KUKU…. Msanii kutoka Ufaransa Abraham Poincheval anaendelea kutamia mayai ya kuku akiwa na matumaini kwamba mwishowe yataangua vifaranga. Msanii huyo anatumia joto kutoka kwa mwili wake kutamia mayao hayo 10. Poincheval amb… Read More
  • CHINA YAPIGA MARUFUKU KUFUGA NDEVU.. Sheria mpya zitaanza kutekelezwa katika jimbo la magharibi mwa Uchina la Xinjiang, ambako utawala wa Beijing unaaendeleza kile wanachokisema ni kuzuia ueneaji wa itikadi kali. Miongoni mwa hatua wanazochukua ni kupiga… Read More
  • IDADI YA WASIO NA CHAKULA DUNIANI YAONGEZEKA- RIPOTI Ripoti mpya kuhusu hali ya janga la chakula duniani imesema idadi ya watu wasio na uhakika wa kupata chakula iliongezeka mwaka jana na kufikia watu milioni 108, ikilinganishwa na milioni 80 mwaka 2015, licha ya jitihada … Read More
  • WATU 250 WAANGAMIA KWENYE MAPOROMOKO.. Mamlaka ya jeshi la Colombia inasema idadi ya waliofariki katika maporomoko ya ardhi nchini humo imefikia watu 250 huku waliojeruhiwa wakiwa 400. Hata hivyo idadi hiyo huenda ikaongezeka kwani bado kuna zaidi ya watu … Read More

0 comments:

Post a Comment