Thursday 2 February 2017

MAHAKAMA YATAKIWA KUFUATILIA DENI LA TRILIONI 7.3…

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametoa wito kwa Mahakama kukusanya Shilingi Trillioni 7.3 ambazo ni matokeo ya serikali kushinda kesi mbalimbali za ukwepaji kodi.

Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya siku ya Sheria na Mwaka mpya wa Mahakama wenye kauli Mbiu isemayo Utoaji haki kwa wakati kuwezesha ukuaji wa uchumi.
Amesema  kuwa Takwimu zinaonyesha kuwa kumekuwa na baadhi ya kesi za pingamizi za kodi ambapo  Serikali imeshinda kesi hizo japo  fedha hizo hazijakusanywa mpaka sasa.
“Kukwepa au kutolipa kodi ni kosa kubwa sana, kila mtu anawajibu wa kulipa kodi nchini kwa maendeleo ya nchi” amesema Dkt Magufuli.
Kwa upande wake Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma amesema kuwa Mahakama imeandaa Mpango mkakati uliolenga kufanya maboresho ndani ya Mahakama.
Naye Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju amesema kuwa Katiba imeanisha bayana Kanuni ambazo zinapaswa kuzingatiwa na Mahakama wakati ikitekeleza mamlaka yake ya utoaji haki.

Siku ya Sheria nchini ilianzishwa mwaka 1996 ikiwa ni siku muhimu ya kuombea Majaji na Mahakimu ili kuweza kusikiliza kesi.

0 comments:

Post a Comment