Wednesday 27 September 2017

TEKSI NDEGE ISIOKUWA NA RUBANI YAZINDULIWA DUBAI…………

Dubai imefanya jaribio la teksi ya kwanza ya ndege isio na rubani ambayo wanatumaini itatumika kama chombo cha uchukuzi mijini.

Ndege hiyo isio na rubani yenye nafasi ya watu wawili iliruka kwa dakika tano katika pwani ya ghuba.
Ndege hiyo ilitazamwa ikipaa angani na mwanamfalme Hamdan bin Mohammed.
Dubai ina malengo makubwa ya kuwa mji wa kiteknolojia huku ndege zisizo na rubani na roboti zikihusika pakubwa katika mpango huo.
Ndege hiyo ya teksi ilibuniwa na kampuni ya Ujerumani ya Volocopter na kampuni hiyo imesema inatumai kwamba ndege hiyo itaanza kufanya kazi katika kipindi cha miaka mitano.
''Utumizi wake utahusisha simu aina ya smartophone, programu na kuagiza ndege hiyo kuruka hadi katika eneo unalopania kuelekea'', alisema Afisa mtendaji wa kampuni hiyo Florian Reuter.
Teksi ndege isiokuwa na rubani awali ilifanyiwa majaribio nchini Ujerumani mnamo mwezi Aprili.
Kampuni pinzani ya China eHand ilitarajiwa kuwa ya kwanza kuzindua msafara wa teksi ndege mjini humo lakini mipango yake ikaonekana kuchelewa.
Dubai imejiweka kuwa mji wa kiteknolojia duniani ikiwa na mipango ya magari ya kujiendesha kusimamia robo ya safari zote kufikia 2030.

Noel Sharkey ambaye ni mwanasayansi wa komyuta na ambaye pia ni mtaalam wa roboti katika chuo kikuu cha Sheffield alisema kuwa: Changamoo kuu itakuwa vikwazo visivyoepukika kama vile kukwepa teksi nyengine, majumba marefu, vindege na ndege zisizokuwa na rubani ambazo zinatumika kusafirisha mizigo.

0 comments:

Post a Comment