Saturday 21 October 2017

GAMBO ATOA AGIZO KWA MKURUGENZI……

Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ameagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Monduli kuhakikisha anasimamia ujenzi wa Ofisi za Kata na unakamilika kabla ya mwezi wa kumi na mbili mwaka huu.

Agizo hilo amelitoa kwenye ziara yake ya siku mbili wilayani Monduli baada ya kujionea juhudi za wananchi wa Kata ya Moita kwa kufanikisha ujenzi wa Ofisi ya Kata kwa nguvu zao wenyewe.
Mkuu huyo wa Mkoa aliahidi kumkabidhi Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo shilingi milioni kumi kwaajili ya kumalizia ujenzi huo ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za wananchi ambao wanajitolea kwaajili ya kujiletea maendeleo yao wenyewe.

Aidha Gambo pia amefanikisha ujenzi wa darasa moja katika shule ya msingi Kilimatinde baada ya kuchangia mabati 60, wakati Wananchi wengine wawili wakatoa milioni 4 kwaajili ya tofali pamoja na mifuko 30 ya Theluji iliyotolewa na Chama cha Mapinduzi wilayani humo.

0 comments:

Post a Comment