Wafanyibiashara
wakubwa Africa, wametakwa kuwa miongoni mwa watu wafisadi zaidi sawa na maafisa
wa polisi Barani Afrika.
Hii ni mara ya kwanza
wafanyibiashara wametajwa kuwa mafisadi wakubwa Barani Africa.
Shirika hili limeongeza kwamba utumizi mbaya wa mamlaka,
unasababisha ongezeko la umasikini, na kuwanyima raia mahitaji muhimu.
Watu wengi ambao ni masikini
wamejikuta mara kadhaa wakilazimika kulipa hongo, ikilinganishwa na matajiri
inasema sehemu ya taarifa hiyo ya Transparency International.
Nchi ya Liberia imetajwa kama nchi inayoongoza kwa visa
vya ufisadi Afrika,inafuatwa na Cameroon, Nigeria na Sierra leone.
Afrika mashariki Uganda inaongoza
kwa visa vya ufisadi, ikifuatwa na Kenya.
Kusini mwa Afrika Zimbabwe na Zambia zinaongoza katika
nchi zenye visa vingi vya ufisadi.
Botswana, Mauritius na Cape
Verde, ndiyo mataifa pekee ya Afrika ambapo visa vya ufisadi ni vya chini zaidi
ikiwa ni asili mia mbili pekee.
0 comments:
Post a Comment