Thursday 31 December 2015

NASA: El Nino hii ni mbaya kama ya 1998..

Hali ya hewa ya El Nino ambayo imekuwa ndiyo kali zaidi katika historia itazidisha hatari ya njaa na maradhi kwa mamilioni ya watu duniani 2016, mashirika ya misaada yamesema.

Hali hii ya hewa inatarajiwa kusababisha ukame baadhi ya maeneo na mafuriko kwingine.
Baadhi ya maeneo yanayotarajiwa kuathirika sana yako Afrika, huku uhaba wa chakula ukitarajiwa kufikia kilele Februari.
Maeneo mengine yakiwemo Caribbea, Amerika ya Kati na Amerika Kusini yataathiriwa katika kipindi cha miezi sita ijayo.
Hali ya hewa ya El Nino, hutokana na kuongezeka kwa joto na huathiri hali ya hewa maeneo mengi. Mwaka huu hali hii imezidi na kuufanya mwaka 2015 kuwa mwaka wenye joto zaidi duniani katika historia.
Kufikia sasa watu 31 milioni wanakabiliwa na uhaba wa chakula Afrika, theluthi moja kati ya hawa wakiwa Ethiopia.
Inakadiriwa kwamba watu 10.2 milioni watahitaji chakua cha msaada mwaka 2016.
Mashirika ya misaada kama vile Oxfam yameelezea wasiwasi kwamba athari za El Nino zitazidisha makali ya mizozo ya sasa kama vile vita Syria, Sudan Kusini na Yemen.
Hali ya hewa ya El Nino inatarajiwa kumalizika katikati mwa mwaka ujao.
Kuna wasiwasi kwamba hali hii huenda ikafuatwa na hali ya La Nina ambayo katika maeneo mengi husababisha ukame.
Hali kama hii ilifuata mvua kubwa 1997/98.

El Nino hutokana na kuongezeka kwa joto baharini nayo hali ya La Nina husababishwa na kushuka kwa viwango vya joto baharini.

0 comments:

Post a Comment