Mbwa wa polisi aliyeuawa wakati wa msako baada ya mashambulio ya Paris, atatunukiwa nishani kuu ya ushujaa.
Diesel mbwa aina
ya Belgian Shepherd mwenye umri wa miaka saba, alifariki wakati wa operesheni
ya kumsaka mshukiwa mkuu wa mashambulio hayo.
Mbwa huyo
atatunukiwa nishani kwa jina Dickin Medal, ambayo hutolewa na shirika la
kuwatunza wanyama la PDSA.
Hadhi ya nishani
hiyo ni sawa na nishani ya Msalaba wa Victoria,inayopewa watu mashujaa vitani.
0 comments:
Post a Comment