Jeshi la
wanahewa la Afrika Kusini limesema kuwa,duma wawili ambao hufugwa kwenye kambi
ya jeshi hilo ili kufukuza wanyama wengine kwenye njia ambayo hutumiwa na ndege
kupaa, wamemshambulia afisa wa jeshi.
Msemaji wa jeshi hilo Marthie Visser amesema kupitia taarifa
kwamba, duma hao waliingia eneo ambalo ndege huegeshwa katika eneo la Makhado.
Mwanajeshi aliyekuwa kwenye zamu aliwaona na kujaribu
kuwapiga picha, na hapo ndipo wakamshambulia.
Mwanajeshi huyo hakujeruhiwa vibaya na ameruhusiwa kutoka
hospitalini,baada ya kupatiwa matibabau.
Hata hivyo uongozi umesema wanyama hao hawatafukuzwa katika
kambi hiyo.
Bi Visser amesema kambi hiyo iliyo kaskazini mwa Afrika
Kusini, imezingirwa na mbuga za wanyama na duma hao husaidia kudhibiti ongezeko
la wanyama mwitu.
0 comments:
Post a Comment