Daktari aliyewaambukiza wagonjwa 200
virusi vya ukimwi nchini Cambodia amehukumiwa jela.
Daktari
huyo bandia alipatikana na hatia ya kuwaambukiza takriban watu 200 virusi vya
ugonjwa wa Ukimwi amehukumiwa kifungo cha miaka 25 jela kwa makosa yake.
Baadhi
ya wahasiriwa wa makosa hayo wamekwisha fariki dunia.
Yem
Chrin alikuwa akitumia sindano zilizokuwa zimekwisha tumika kuwatibu wenyeji wa
kijiji cha Roka bila ya kujua alikuwa akisambaza Virusi vya Ukimwi.
Awali
Chrin alikuwa ameshtakiwa kwa mauaji, lakini upande wa mashtaka ukabadilisha
shtaka na kuwa kuua bila ya kukusudia.
Kesi hiyo imefichua
uhaba wa madaktari na ugumu ulioko kwa raia kupata huduma za afya katika maeneo
mengi ya vijijini nchini Cambodia.
Utafiti
umebaini kuwa zahanati nyingi katika maeneo ya vijijini, huendeshwa na
madakatari bandia ambao hawajahitimu kuwatibu wagonjwa.
0 comments:
Post a Comment